Miili yetu inahitaji chumvi kiasi kidogo sana. Kwa wastani tunahiaji kama gramu 1.25 (kama robo kijiko cha chai) kwa siku. Kwa bahati mbaya tunatumia chumvi kupita kiasi. Wataalamu wa Afya wanahusisha matumizi ya chumvi nyingi na uwezekano wa kupata msukumo mkubwa wa damu (High Blood Pressure), ambayo pia inaongeza uwezekano wa kupata magonjwa mengine sugu kama yale ya figo, moyo, ikiwepo “stroke” na pia ya mifupa kama “osteoporosis”.
Hivi karibuni tafiti zimeonyesha uhusiano mkubwa kati ya matumizi ya vyakula vyenye chumvi nyingi na saratani ya tumbo.
Tagged as: Chumvi






