Nafaka zisizokobolewa (whole grains), aina mbali mbali za kunde na maharage (legumes) zimeonekana kuupa mwili afya bora na faida nyingi sana ikiwepo kuzuia baadhi ya saratani (cancer).  Tujizoeshe kula na tufurahie kula vyakula hivi.  Nafaka zisizokobolewa ni kama unga wa dona, mkate wa brauni (uliotengenezwa na ngano ambayo haikukobolewa sana), mchele wa brauni na ulezi, pia mtama (sorghum) au uwele ambao haukukobolewa. Jamii za mikunde zinahusisha maharage, kunde, mbaazi, njugu mawe, choroko, fiwi, dengu, njegee kavu nk.

(more…)

del.icio.us Digg Facebook Google Twitter Mail to a friend Thank you for sharing!